Skip to main content

Chapati laini za maziwa



Mahitaji
1.     Unga wa Ngano-1 kg
2.     Mafuta ya kupikia ya vuguvugu kwa ajili ya kukandia ½ kikombe na ¼ kikombe kwa ajili ya kuchomea
3.     Chumvi kijiko cha chakula 1
4.     Sukari Vijiko 3 vya chakula
5.     Maziwa ya vuguvugu au waweza tumia maji ya vuguvugu

Vifaa
      i.        Ubao wa kusukumia chapati na mpini wake
     ii.        Frying pan flat na Mwiko wa kugeuzia chapati
    iii.        Bakuli kubwa kwa ajili ya kukandia unga
    iv.        Sehemu safi flat kwa ajili ya kukandia unga


Instructions/Maelekezo
1.     Mimina Unga kwenye bakuli ya kukandia, mimina chumvi, mimina sukari pia kasha changanya vizuri.
2.     Mimina mafuta ya vuguvugu kwenye bakuli ya unga halafu changanya vizuri kuondoa crumps
3.     Anza kumimina maziwa ya vuguvugu kidogokidogo, kwenye unga huku ukiwa una changanya unga na maziwa ushike vizuri, mimina maziwa mpaka pale unga utakapokuwa tayari kukandwa.
4.     Kanda unga wako kwenye bakuli, mpaka uone unaanza kulainika, waweza kukandia kwenye flat surface ukiwa unauvuta vuta na kukanda vizuri mpaka uone unga haunati kwenye mikono hapo unga wako utakuwa tayari umekandika.
5.     Baada ya kukanda  pakaza mafuta kwenye bakuli (waweza tumia sponge au brush) halafu weka dough kwenye bakuli yako kisha funika na kitambaa safi. Acha utulie kwa dk 10 hivi.
6.     Bada ya dk 10, toa dough kwenye bakuli anza kukata miduara size ambayo utasukumia chapatti (angalia picha)
7.     Nyunyiza unga kidogo sehemu ya kusukumia chapatti, sukuma maduara shape ya chapatti kisha, pakaza mafuta upande mmoja wa chapatti then viringisha (angalia picha), hapa fanya hvyo kwa maduara yote, kisha panga miviringo yako kwenye sinia ulilonyuniza unga. Funika acha kwa dk 5.
8.     Baada ya dk 5, anza kuandaa kuchoma chapatti
9.     Weka flat skillet kwenye moto wa wastani, acha ipate moto, kisha nyunyiza unga kidogo kwenye ubao wa chapati, sukuma chapati iwe na shape ya chapati kisha weka kweye frying pan ya moto uanze kuchoma.
10.  Acha chapati ipate joto kisha geuza chapati upande wa pili ipate joto hapo ndo uweke mafuta kidogo, halafu ugeuze geuze chapati hadi iive vizuri rangi ya golden brown, toa chapati weka kwenye sahani au hot pot. Fanya hivyo kwa maduara yote yalobaki mpaka umalize.

Chapati zitakua tayari waweza kula kama dinner na maharage, roast ya nyama, au hata asubuhi kwa ajili ya kitafunwa.

NB: Ili upate chapate laini hutakiwi kuwa na haraka kwenye kukanda, waweza tumia muda mrefu kwenye kukanda mpaka dough iwe laini na isiyoshikana na mikono yako.


Maelekezo ya picha bonyeza hapa

Comments

Popular posts from this blog

NJIA RAHISI YA KUTENGENEZA KEKI YA VANILLA

Jinsi ya Kupika Visheti/Vikokoto~Crunchy Visheti

Half Cake za maziwa